• Nairobi
  • Last Updated May 19th, 2024 9:01 PM
Karen Nyamu anavyotumia msanii Samidoh kuvuna umaarufu kisiasa   

Karen Nyamu anavyotumia msanii Samidoh kuvuna umaarufu kisiasa  

NA SAMMY WAWERU

SENETA maalum Karen Nyamu anaendelea kupata umaarufu, hasa kutokana na uhusiano wake kimapenzi na mwanamuziki wa Mugithi, Samuel Muchoki, ‘Samidoh’. 

Wamejaaliwa kupata watoto wawili, licha ya kuwa Samidoh ni mume na baba.

Ni kufuatia uhusiano haramu kati yao, mkewe Edday Nderitu Mei 2023 alisafiri Amerika kwa minajili ya likizo.

Likizo hiyo, hata hivyo, iligeuka kuwa fursa ya Edday kuhamia nchini humo.

Amepewa makazi na bintiamu wa Samidoh, Bernice Saroni ambaye kulingana na maelezo yake ya utambuzi mitandaoni anaishi Lowell, Massachusetts.

Julai 2023, Edday alithibitisha kwamba amemtema Samidoh, kufuatia udanganyifu wake kwenye ndoa.

Mapema 2023, mama huyo wa watoto watatu alitoa tahadhari kuhusu uhusiano wa msanii huyo na Karen Nyamu, akisema “sitavulia kuishi na mume anayeenda nje ya ndoa”.

Samidoh na Karen, wamekuwa kwenye mahusiano haramu tangu 2020.

Huku Karen akiwa jasiri kuelezea bayana ‘mapenzi yake ya dhati’ kwa mwimbaji huyo mitandaoni, imebainika kwamba mwanasiasa huyo wa chama cha UDA anatumia umaarufu wa Samidoh kusaka kiti cha kisiasa 2027.

“Analenga kuwania kiti cha mbunge mwakilishi wa wanawake Nyandarua,” Taifa Leo Dijitali imearifiwa na mmoja wa wandani wa familia ya Samidoh, aliyeomba kubana majina yake.

Uchaguzi mkuu 2017, Karen aliwania wadhifa wa mwakilishi wa kike Nairobi kupitia chama cha Jubilee japo alishindwa na Esther Passaris wa ODM.

Passaris anahudumu muhula wa pili.

Kulingana mjuzi wetu, Karen anapanga mahesabu ya siasa kwa kutumia jukwaa la umaarufu wa msanii Samidoh.

“Ndio maana Karen amekuwa akiandamana na Samidoh katika ziara kadha Nyandarua kusambaza chakula cha msaada kwa familia zisizojiweza,” akaelezea.

Muimbaji huyo wa kibao maarufu cha ‘Kairitu Gakwa’ ameonekana mara kadha hadharani na seneta Karen.

Katika kile kilionekana kama ‘kulinda mumewe’, Desemba 2022 Karen alivamia kilabu kimoja Dubai ambapo Samidoh alikuwa ameandamana na Edday Nderitu kutumbuiza mashabiki wake.

Mabaunsa walilazimika kutuliza mwanasiasa huyo, Samidoh akihepa drama na mkewe ambaye ametangaza kumpa talaka.

Duru pia zinaarifu, mwanamuziki huyo ambaye pia ni askari huenda akawania kiti cha kisiasa 2027.

  • Tags

You can share this post!

Wanasiasa wageuza mjadala kuwa mzaha

MCA sasa ndio wafalme na malkia wapya vijijini

T L