• Nairobi
  • Last Updated May 19th, 2024 10:50 AM
Karen Nyamu anunulia Samidoh pombe ya bei ghali kusherehekea Sikukuu ya kina Baba

Karen Nyamu anunulia Samidoh pombe ya bei ghali kusherehekea Sikukuu ya kina Baba

Na SAMMY WAWERU

SENETA maalum Karen Nyamu amenunulia ‘mchumba wake’ Samuel Muchoki ‘Samidoh’ pombe ya kima cha Sh420, 000 kuadhimisha Sikukuu ya kina Baba Duniani.

Kupitia video inayosambaa mitandaoni, Bi Karen anaonekana akiingia katika mojawapo ya maduka ya kuuza vileo jijijini Nairobi akieleza wahudumu “ninataka pombe ya bei ghali kununulia mubaba wangu”.

Akiwa amevalia sweta nyekundu, suruali ndefu – long’i nyeusi na chepeo ya rangi nyeupe, seneta huyo wa chama cha UDA anaingia katika duka hilo akitembea kwa madaha.

“Nimekuja kununulia mbabas pombe ya Father’s day,” mwanasiasa huyo anaskika akisema.

Anakaribishwa na mhudumu wa kike, na kupiga maraundi kwenye duka hilo.

“Nataka ile ya doo mob kabisa, ile ya bei ghali,” anasisitiza.

Mhudumu anamuorodheshea na kumtajia mseto wa vileo, ikiwemo ya Sh420, 000 na S210, 000.

“Hii (Ya Sh420, 000) ndiyo bei ghali sana,” mhudumu anamwambia.

Karen anainunua, na kupakiwa kisha anafululiza kwenye gari lake la rangi jeupe lililoegeshwa nje.

Sikukuu ya kina Baba ulimwenguni huadhimishwa Juni 18 kila mwaka.

“Siku ya furaha ya kina Baba kwa baba nzuri wa watoto wetu wote. Una roho ya utu na mkarimu. Leo (Jumapili, Juni 18, 2023) tunakusherehekea na ujue tunakudhamini kufuatia furaha unayotuletea,” Karen Nyamu akaandikia kupitia Instagram.

Seneta huyo vilevile alipakia video ya Samidoh akiwa na mvulana wake mdogo, aliyepata pamoja na msanii huyo.

Samidoh ambaye ni mwimbaji wa nyimbo za Mugithi, amekuwa kwenye mahusiano haramu na mwanasiasa huyo licha ya kuwa mume wa Edday Nderitu.

Samidoh na Edday wana watoto watatu pamoja, na Mei 2023 mkewe huyo alisafiri Amerika kwa minajili ya likizo.

Hata hivyo, imebainika kuwa Edday huenda akakosa kurejea nchini jambo ambalo linaashiria mwisho wa ndoa yake ya miaka 15.

Mapema 2023, Edday alichapisha kupitia ukurasa wake rasmi wa Facebook ghadhabu zilizoonyesha kuchoshwa na tabia za mumewe kuwa na mahusiano haramu na Karen Nyamu.

Seneta Karen na Samidoh wana watoto wawili pamoja.

  • Tags

You can share this post!

Wagemaji chang’aa Murang’a waomba kuruhusiwa kutumia...

Genge linaloiba mifugo Murang’a na kuacha kinyesi cha...

T L