• Nairobi
  • Last Updated May 19th, 2024 10:50 AM
Karen Nyamu: Harusi nyingine ya Akothee ikifanyika tutadensi vilivyo

Karen Nyamu: Harusi nyingine ya Akothee ikifanyika tutadensi vilivyo

NA MWANDISHI WETU

SENETA maalum Karen Njeri Nyamu ameeleza kuwa atakuwepo kwenye harusi ya mwanamuziki Esther Akoth almaarufu Akothee endapo atafanya nyingine.

Kupitia ujumbe wake mtandaoni alipokuwa akimjibu mmoja wa wa wafuasi wake, Bi Nyamu alisema ikifanyika atasakata rumba ipasavyo.

“Njeri hadi mkadensi harusi ya Omosh,” akaandika Lucy Kibunja.

Nyamu alimjibu: “Hata hiyo nyingine tutadensi kwanza sana.”

Bi Nyamu ni mmoja wa waalikwa wa harusi ya Akothee na Omosh iliyofanyika Aprili 10, 2023 katika hoteli ya kifahari ya Windsor Golf.

Hata hivyo, sio tu Bi Nyamu ambaye ametangaza kuwepo katika harusi nyingine ya Akothee, mcheshi Sande Bush almaarufu Dr Ofweneke alieleza kuwa lazima atakuwa mfawidhi (MC) katika sherehe hiyo.

Kwenye ukurasa wake, Dr Ofweneke aliandika, “Hata ufanye harusi ngapi nitakuwa hapa na wewe. Leta mzungu mwingine.”

Kwa upande wake, Akothee alijibu, “Wa nane anakuja…Ochise wa 8.”

Inadaiwa kuwa mwanamuziki huyo alitengana na mumewe Denis Schweizer almaarufu Omosh miezi kadhaa baada ya kufunga ndoa.

Licha ya kiini chake kutojulikana, wanamitandao wanakisia kuwa Bw Schweizer alikuwa na familia nyingine ambayo aliiweka siri.

Hata ingawa Akothee hajafunguka kuhusu kilichoenda mrama kwenye ndoa yake, alishatoa jina la Bi Schweizer alilokuwa ameweka kwenye uso wa ukurasa wake wa Instagram.

Isitoshe, akaunti ya Bw Omosh kwenye mtandao huo wa kijamii umekwisha kuondolewa.

 

  • Tags

You can share this post!

Bloga ashtakiwa kwa kuchapisha habari za uongo kuhusu Naibu...

SHINA LA UHAI: Uhaba wa dawa za TB wahatarisha afya ya...

T L