• Nairobi
  • Last Updated May 3rd, 2024 7:50 PM
MAPISHI KIKWETU: Chipsi masala zilizo na kitunguu saumu na bizari nyembamba

MAPISHI KIKWETU: Chipsi masala zilizo na kitunguu saumu na bizari nyembamba

NA MARGARET MAINA

[email protected]

Muda wa kuandaa: Dakika 15

Muda wa mapishi: Dakika 30

Walaji: 2

Vinavyohitajika

viazi mbatata

vitunguu maji 2 vilivyokatwa

kikombe ½ cha dania iliyokatwakatwa

punje 5 za kitunguu saumu ambapo unakata vipande

kijiko 1 cha tangawizi ya kusaga

pilipili

vijiko 5 nyanya ya kopo

kijiko ¼ cha manjano

kijiko ¼ cha bizari nyembemba

kijiko ¼ cha paprika

gramu 125 za jibini ya mozzarella

kikombe ¼ cha bekoni iliyopikwa ikakatwa

majani ya giligilani kwa ajili ya kupamba

Maelekezo

Anza kwa kuandaa viazi. Menya na katakata halafu kaanga viazi kisha uviwekae kando.

Ili kuandaa mchuzi, anza kwa kupika vitunguu, mashina ya dania, kitunguu saumu na tangawizi kwenye mafuta ya bekoni hadi vilainike na viwe na harufu nzuri.

Mashina ya dania ni kiungo bora na hufanya kama nyongeza ya ladha tamu katika hatua za awali za kupikia.

Ongeza nyanya ya kopo, viungo na maji kidogo ya moto na kuruhusu hii kupika hadi nzito na yenye ladha.

Nenda kwa urahisi juu ya maji, kusudi lake ni kuwezesha kupikia tu viungo sio kutengeneza supu.

Ongeza kwenye viazi na kuchanganya. Kuwa mpole na hakikisha usibonde.

Pamba kwa majani ya gilgilani na kisha pakua. Unaweza kuzifurahia chipsi zako katika hatua hii, lakini unaweza kuongezea jibini ya mozzarella uliyoyeyusha na bekoni pia.

  • Tags

You can share this post!

Polisi wachunguza tukio la raia wa Misri kutekwa nyara...

Vyakula vilivyo na vitamini E ambayo ni muhimu kwa ngozi na...

T L