• Nairobi
  • Last Updated May 4th, 2024 6:55 AM
Ole wako endapo ulikuwa unamezea mate Mulamwah, amefanya harusi

Ole wako endapo ulikuwa unamezea mate Mulamwah, amefanya harusi

NA FRIDAH OKACHI

NI rasmi sasa mcheshi na mwanakotenti David Oyando maarufu kama Mulamwah, ameondokea maisha ya upweke baada ya kufanya harusi ya kitamaduni na mchumba wake Ruth Wambui.

Harusi hiyo ilifanyika Jumamosi, Oktoba 28, 2023 katika eneo ambalo limesalia kuwa fiche.

Ruth almaarufu Ruth K wakati mwingi amekuwa akitambulishwa kama ‘bestie’ na Mulamwah.

Hafla ya Mulamwah na kipenzi chake kufunga ndoa, ilifichuka kupitia picha zilizochapishwa na Ruth kwenye akaunti yake rasmi ya Instagram.

Ruth alionekana amevalia kitenge maridadi, naye Mulamwah akiwa amevalia mavazi ya kijani.

Ruth pia alipakia video iliyoonyesha bango lenye maandishi ‘Karibu kwenye sherehe ya kitamaduni yake David na Ruth’.

Baadaye, Mulumwah kupitia Instagram alichapisha ujumbe na picha, kudhihirisha sherehe hiyo inaendelea.

“Leo nimefika nyumbani kwa kina bestie,” aliandika mcheshi huyo.

Sherehe hiyo ilihudhuriwa na familia na marafiki wa karibu, ambao walionekana kufurahia wawili hao wakifunga ndoa.

Baadhi ya wasanii na waigizaji tajika walionekana katika hiyo.

“Leo nimekuwa kwa harusi ya Mulamwah,” alichapisha msanii Jacky Vicky maarufu Awinja.

Siku kadha zilizopita, Mulamwah kupitia Instagram alidokeza kwamba mpenziwe, Ruth K ni mjamzito.

Alielezea matumaini kwamba hivi karibuni wanatarajia kupata mtoto.

“Bestie amekuwa akitapika majira ya asubuhi, ishara kuwa ana mimba.”

Kabla ya kukutana na Ruth K, Mulamwah alikuwa kwenye mahusiano na mwanakontenti Carol Sonnie na walijaaliwa kupata mtoto mmoja.

Sonnie anaonekana kutofurahishwa na tangazo la Mulamwah, mpenziwe Ruth K kuwa mjamzito.

Hilo lilidhihirika baada ya shabiki wa msanii huyo kumtaja Sonnie kwenye chapisho hilo, ashuhudie kinachoendelea.

“Bestie ana mimba na huyu mwingine si wake?” Sonnie alichapisha.

Awali, Mulamwah alikuwa amekana kwamba yeye si baba wa mtoto wa Sonnie.

Msanii huyo na Ruth K wamekuwa wakikana kuwa kwenye mahusiano hadi mwaka huu, 2023 siku maalum ya wapendanao ambapo waliweka wazi kuwa kitu kimoja.

 

  • Tags

You can share this post!

Mwanamume apatikana ameuawa na mwili kutupwa mtoni...

Matunda ya Gachagua kuboresha sekta ya kahawa yaanza...

T L