• Nairobi
  • Last Updated May 21st, 2024 11:37 AM
Mwanamume apatikana ameuawa na mwili kutupwa mtoni Kirinyaga   

Mwanamume apatikana ameuawa na mwili kutupwa mtoni Kirinyaga  

NA GEORGE MUNENE

MWANAMUME mmoja amepatikana ameuawa na mwili wake kutupwa katika mto Rwamuthambi katika Kaunti ya Kirinyaga.

Mwili wa mwendazake uligunduliwa na wavulana wawili ambao walikuwa wameenda kuogelea katika mto huo Ijumaa jioni, Oktoba 27, 2023.

Wavulana hao walipiga kamsa, na kuvutia wakazi waliopiga ripoti kuhusu kisa hicho kwa polisi.

Muda mfupi baadaye, polisi walifika na kuopoa mwili huo na kuupeleka katika hifadhi ya maiti kufanyiwa upasuaji.

Wakazi wanashuku kuwa mwanamume huyo ambaye hajatambuliwa aliuawa na wahalifu kisha mwili wake utakupwa mtoni kuzima ushahidi.

 

  • Tags

You can share this post!

Lupita sasa aamua kufuga paka baada ya kutemwa

Ole wako endapo ulikuwa unamezea mate Mulamwah, amefanya...

T L