NA MWORIA MUCHINA
SIAFU anayefahamika kwa Kiingereza kama ‘bullet ant’ akikuuma utahisi uchungu kama mtu aliyepigwa risasi.
Sumu ya siafu hawa inafanyiwa utafiti na wanasayansi kugundua kama inaweza kutengeneza dawa ya kuua wadudu waharibifu.
Kwa mujibu wa mila na desturi za kabila la Mawé linalopatikana kwenye msitu wa Amazon nchini Brazil, mwanamume kamili ni yule anayevumilia kuumwa na siafu hao. Mwanamume anapoumwa na siafu hao ni sharti avumilie kwa kutofunga jicho au kulalamikia uchungu.?