• Nairobi
  • Last Updated May 19th, 2024 10:50 AM
PATA USHAURI WA DKT FLO: Nitakabili vipi ‘allergy’ ya maziwa kwa mwanangu?

PATA USHAURI WA DKT FLO: Nitakabili vipi ‘allergy’ ya maziwa kwa mwanangu?

Mpendwa Daktari,

Nitakabiliana vipi na tatizo la mzio wa maziwa linalomkumba mtoto wangu?

Jayson, Mombasa

Mzio wa chakula ni tatizo la kawaida ambalo hukumba angalau kila mmoja wakati mmoja maishani. Mzio kamili wa chakula ni mwitikio usio wa kawaida katika mfumo wa kinga mwilini baada ya kula chakula fulani.

Mzio wa chakula hujitokeza kwenye vyakula ni viungo ambavyo huchochea mzio mwilini. Kwa wingi viungo hivi huwa protini zinazokinza moto wakati wa upishi, asidi kwenye tumbo na vimeng’enya tumboni. Allergen hizo hudumu kwenye ukuta wa utumbo, kuingia kwenye mfumo wa damu na kulenga viungo fulani mwilini na hivyo kusababisha mzio (allergy).

Mara nyingi mzio mwingi wa chakula hutokea katika kipindi cha mwaka mmoja au miwili ya kwanza ya mtoto. Japo mzio mwingine wa vyakula kama maziwa na mayai huisha mtoto anapozidi kukua, kuna mwingine ambao huendelea maishani. Litakuwa jambo la busara kumpeleka mwanao hospitalini ili achunguzwe vilivyo.

Kumbuka kwamba kumnyonyesha mtoto pekee pasipo kumlisha chakula kingine katika miezi minne ya kwanza maishani husaidia kupunguza uwezekano wa kukumbwa na mzio wa maziwa katika miaka miwili ya kwanza.

You can share this post!

DALILI NZURI: Maumivu na uchovu ni ishara chanjo inafanya...

AFC: Wasiwasi kambini kuhusu kocha Aussems