• Nairobi
  • Last Updated May 8th, 2024 7:50 AM
UDAKU: Jicho kali la nje laponza kocha mwenye tamaa ya fisi

UDAKU: Jicho kali la nje laponza kocha mwenye tamaa ya fisi

Na CHRIS ADUNGO

IMEFICHUKA kwamba jicho kali la nje ndicho kiini cha kocha Paul Riley kupoteza posho aliyokuwa akipokezwa na klabu ya North Carolina Courage.

Riley, 58, alipigwa kalamu wiki iliyopita kwa madai ya kuwadhulumu kimapenzi vipusa wa kikosi hicho cha Ligi Kuu ya Soka ya Wanawake Amerika (NWSL).

Madai dhidi ya mkufunzi huyo raia wa Uingereza yaliwekwa wazi kupitia taarifa iliyochapishwa na gazeti la The Athletic Alhamisi iliyopita.

Kufichuka kwa habari hizo kulichochea Shirikisho la Soka Amerika kumpokonya Riley leseni ya ukocha na kupendekeza atimuliwe mara moja.

Riley alizaliwa jijini Liverpool, Uingereza, na akaanza taaluma ya ukufunzi nchini Amerika mnamo 1986.

Anatuhumiwa kulazimisha wanasoka wa kikosi chake kumfungulia mizinga ya asali nyakati mbalimbali.

Ripoti ya The Athletic ilichapisha maelezo ya baadhi ya wachezaji walioungama kuwahi kudhulumiwa kimapenzi waliponolewa na Riley, ambaye alihudumu katika ligi ya NWSL tangu 2014.

Miongoni mwa vipusa hao ni Mana Shim na Sinead Farrelly, aliyewahi kutiwa makali na Riley kambini mwa Philadelphia Independence (2011), New York Fury (2012) na Portland Thorns (2014-2015).

“Riley alivutiwa sana na warembo wenye ghuba kubwakubwa na maziwa yaliyosimama tisti vifuani. Ilitokea kwamba nilikuwa katika kundi la vidosho hao, na alilimenya tunda kwa lazima kwa mara ya kwanza mnamo 2011,” akaeleza Farrelly kwenye mahojiano na The Athletic.

Riley amesimamia vikosi kadhaa vya soka ya wanawake nchini Amerika tangu 2006.Ingawa amekana madai hayo, Shim ameungama kuwa kocha huyo aliwahi pia kumtambalia mara kadhaa kati ya 2019 na 2020.

“Ilinichukua muda kugundua kwamba alikuwa akiwania buyu la karibu kila mchezaji kikosini, na kila aliyemnyima aliozea benchi,” akasema.

Kidosho mwingine aliyeviziwa na Riley kambini mwa North Carolina Courage aliripoti tukio hilo kati ya Aprili na Julai mwaka huu, japo alitaka isalie kuwa siri.

“Tumebana jina lake sababu tunaheshimu haki zake na tunatambua kwamba suala hili limemwathiri kisaikolojia,” ikasema The Atheltic na kukiri kuwa Riley alimbaka mchezaji huyo katika hoteli moja ya kifahari jijini Los Angeles.

“Alinijia baada ya juhudi za kumlaza kipusa mwenzangu kikosini kuambulia pakavu. Alichovya asali kwa lazima na muda haukupita kabla yake kudandia mwanafasheni mwingine maarufu raia wa Amerika,” aliungama kichuna huyo.

Kikosi cha North Carolina Courage kimepongeza wanasoka wake kwa ujasiri wa kufichua uozo wa Riley na kuahidi kushirikiana na vinara wa NWSL kuendeleza uchunguzi zaidi.

You can share this post!

DIMBA NYANJANI: Amazon Tigers shabaha yao kunogesha Ligi...

DIMBA: Ramsdale ‘nyani’ mpya asiyecheka na mtu...