• Nairobi
  • Last Updated May 19th, 2024 6:50 AM
TUSIJE TUKASAHAU: Serikali imezembea kufanikisha utekelezaji wa Sheria ya Udhibiti wa Tumbaku ya 2007

TUSIJE TUKASAHAU: Serikali imezembea kufanikisha utekelezaji wa Sheria ya Udhibiti wa Tumbaku ya 2007

WATAALAMU wa afya wanakubaliana kwamba uvutaji sigara unasababisha madhara ya kiafya hususan ugonjwa wa kansa ya mapafu.

Nchini Kenya uraibu huu unahusishwa na zaidi ya asilimia 70 ya maradhi ya kansa ya mapafu, kulingana na Mwongozo wa Kitaifa kuhusu Udhibiti wa Kansa.

Lakini licha ya hatari hii, Wizara ya Afya inayoongozwa na Mutahi Kagwe na Wizara ya Usalama yake Fred Matiang’i zimeonekana kuzembea katika wajibu wao wa kufanikisha utekelezaji wa Sheria ya Udhibiti wa Tumbaku ya 2007 inayopiga marufuku uvutaji sigara hadharani.

Uchunguzi wa safu hii umeibaini kuwa waraibu wa sigara wamerejelea mwenendo wa zamani wa kuvuta sigara hadharani au maeneo ya umma, hali inayohatarisha maisha ya wananchi.

Mawaziri hawa wasije wakasahau kuwa wizara zao zina wajibu wa kufanikisha na kudumisha utekelezaji wa sheria hii ya udhibiti wa matumizi ya bidhaa za tumbaku.

You can share this post!

Oparanya aeleza kwa nini aliachia Raila nafasi

Serikali na wanasiasa wajitia hamnazo njaa ikiua wakazi...

T L