Na MASHIRIKA
AC Milan walipoteza fursa ya kupaa hadi kileleni mwa jedwali la Ligi Kuu ya Italia (Serie A) baada ya kulazimishiwa sare ya 1-1 na mabingwa watetezi Inter Milan.
Hakan Calhanoglu aliwaweka Inter kifua mbele kupitia penalti mwanzoni mwa kipindi cha kwanza kabla ya wenyeji Milan kusawazishiwa na Stefan de Vrij aliyejifunga katika dakika ya 17. Penalti ya Lautaro Martinez wa Inter ilipanguliwa na kipa wa Milan kabla ya Alexis Saelemaekers na Franck Kessie kupoteza nafasi za wazi za kuwaweka Milan kifua mbele.
Zlatan Ibrahimovic alishuhudia pia mpira wake wa ikabu ukipanguliwa na kipa Samir Handanovic wa Milan ambao kwa sasa wanashikilia nafasi ya pili jedwalini kwa alama 32 sawa na viongozi Napoli waliolazimishiwa sare ya 1-1 na Hellas Verona.
Inter wanakamata nafasi ya tatu kwa pointi 25, tatu nyuma ya Atalanta wanaofunga orodha ya nne-bora.