• Nairobi
  • Last Updated May 20th, 2024 1:20 PM
AFC Leopards youth yateleza ligi ya NWRL

AFC Leopards youth yateleza ligi ya NWRL

Na JOHN KIMWERE
MATUMAINI ya AFC Leopards Youth kusajili alama tatu kwenye mechi za Kundi A kuwania taji la Nairobi West Regional League (NWRL) yaligonga ukuta ilipolazwa mabao 2-0 na Makarios 111 (Riruta United) ugani Riruta Stadium, Nairobi.
Kwenye matokeo hayo, 360 Media FC ilicharaza Silver Bullets bao 1-0 na kuendelea kukaa kileleni mwa jedwali la kipute hicho. Wasomi hao chini ya nahodha, Jamal Jamaa walionyesha soka safi na kufanikiwa kufunga bao hilo kupitia juhudi zake Fidelis Sennah.
Makarios ya kocha, Geoffrey ‘Jombe’ Osoro ilizima jitihada za AFC Leopards kupitia Billy Rading na December Kisakah. ”Tunashukuru wachezaji wetu kazi nzuri waliofanya kwenye mchezo huo huku tukitoa wito wajitahidi kwenye mechi zijazo,” meneja wa Makarios, Josphat Karuri alisema na kuongeza kuwa hawana jingine bali wamepania kubeba tiketi ya kupandishwa ngazi kushiriki Ligi ya Taifa Daraja la Pili muhula ujao.
Kwenye mfululizo wa matokeo hayo, Fortune Makabwa alicheka na wavu mara moja na kubeba Kibera Golden kushinda maafande wa Nairobi Prisons kwa bao 1-0. Nayo Reunion FC ilijituma kwa udi na uvumba na kulazimisha kutoka nguvu sawa mabao 2-2 na South B United wafungaji wa Reunion walikuwa Ibrahim Omondi na Dickson Gitae.
Douglas Omwenga alitikisa wavu mara mbili na kusaidia Amazon Tigers kuangusha Uthiru Vision kwa mabao 2-1. Bao la Uthiru lilifunikwa kimiani na Kimathi Dancun. Kutokana matokeo hayo, 360 Media FC ingali kifua mbele kwa kufikisha alama 49, nne mbele ya AFC Leopards Youth.
Makario imefunga tatu bora kwa kusajili pointi 44, mbili mbele ya Amazon Tigers
  • Tags

You can share this post!

Wakulima walalamikia kanuni mpya za miwa

Raila amezea mate OKA