• Nairobi
  • Last Updated May 5th, 2024 6:50 AM
Alexis Sanchez aongoza Olympique Marseille kung’oa PSG kwenye raundi ya 16-bora ya French Cup

Alexis Sanchez aongoza Olympique Marseille kung’oa PSG kwenye raundi ya 16-bora ya French Cup

Na MASHIRIKA

MSHAMBULIAJI wa zamani wa Arsenal, Manchester United na Inter Milan, Alexis Sanchez, alifunga bao na kusaidia waajiri wake Olympique Marseille kudengua Paris Saint-Germain (PSG) ambao ni mabingwa mara 14 wa French Cup, kwenye kipute hicho kwa mabao 2-1 mnamo Jumatano usiku.

Sanchez aliwaweka wenyeji Marseille kifua mbele kupitia mkwaju wa penalti katika dakika ya 31 baada ya Sergio Ramos kumwangusha Cengiz Under ndani ya kijisanduku.

Ingawa Ramos alisawazisha mambo mwishoni mwa kipindi cha kwanza, Marseille walifunga bao la ushindi kunako dakika ya 57 kupitia kwa fowadi matata raia wa Ukraine, Ruslan Malinovskyi.

Japo PSG waliwajibisha Lionel Messi na Neymar katika pambano hilo, vigogo hao walishindwa kutambisha waajiri wake katika mechi hiyo ya raundi ya 16-bora.

Marseille, ambao kwa sasa wanakamata nafasi ya pili katika Ligi Kuu ya Ufaransa (Ligue 1) kwa alama 46, nane nyuma ya viongozi PSG, walijizolea taji la French Cup mara ya mwisho mnamo 1988-89.

Vikosi hivyo viwili vitakutana tena mnamo Februari 26, 2023 katika mchuano wa Ligue 1.

TAFSIRI NA: CHRIS ADUNGO

  • Tags

You can share this post!

Pigo kwa Spurs jeraha la goti likitarajiwa kumweka mkekani...

Je, kuna chakula cha kukusaidia usizeeke haraka?

T L