• Nairobi
  • Last Updated May 18th, 2024 8:57 PM
Antony anayekabiliwa na tuhuma za kuwadhulumu wanawake kukosa mechi ya Man-U dhidi ya Crystal Palace

Antony anayekabiliwa na tuhuma za kuwadhulumu wanawake kukosa mechi ya Man-U dhidi ya Crystal Palace

NA AFP

LONDON, UINGEREZA

WINGA wa klabu ya Manchester United, Antony, anatarajiwa kujiunga na wenzake kambini kwa mazoezi huku akiendelea kushirikiana na polisi wanaochunguza madai yanayomwandama ya udhalilishaji wanawake, klabu imetangaza Ijumaa.

Staa huyo raia wa Brazil, ambaye amekanusha vikali madai hayo, alipewa likizo na Man-U mnamo Septemba 10.

Alirejea nchini Uingereza mapema wiki hii na akajipeleka kwa hiari kuhojiwa na Polisi wa Greater Manchester jana Alhamisi.

Man-U wamethibitisha winga huyo mwenye umri wa miaka 23 anarejea kwa mazoezi kwa nia moja tu ya kumridhisha kocha Erik ten Hag.

Ingawa hivyo, hatakuwa sehemu ya kikosi kitakachowajibishwa kwenye mpambano wa EPL ambapo ‘Mashetani Wekundu’ watakwaruzana na Crystal Palace ugani Old Trafford.

“Tangu madai hayo yaibuke Juni 2023, Antony amekuwa akishirikiana na polisi nchini Brazil na Uingereza, na anaendelea kufanya hivyo. Tunapinga dhuluma za aina yoyote,” taarifa ya Man-U imesema.

Antony inadaiwa alimuumiza mpenzi wake wa zamani, Gabriela Cavallin, aliyepasha vyombo vya habari nchini Brazil mapema mwezi huu wa Septemba.

Winga huyo amekanusha madai hayo na ya wanawake wengine wawili.

Antony alijiunga na Man-U akitokea Ajax mwaka 2022 kwa dau la dola milioni 101.

Amefunga mabao manane tu kwa mechi 48.

  • Tags

You can share this post!

Mwanamume ashtakiwa kwa kumuua mzazi sababu ya...

Cherargei akashifu tena Ababu, mara hii kuhusu mwanariadha...

T L