• Nairobi
  • Last Updated May 18th, 2024 8:57 PM
Barcelona wafaulu kumng’oa beki Marcos Alonso kambini mwa Chelsea

Barcelona wafaulu kumng’oa beki Marcos Alonso kambini mwa Chelsea

Na MASHIRIKA

BARCELONA wamejinasia huduma za beki wa kushoto raia wa Uhispania, Marcos Alonso, 31, aliyebanduka Chelsea akiwa na mwaka mmoja zaidi kwenye mkataba wake ugani Stamford Bridge.

Nyota huyo amesajiliwa kwa kandarasi ya mwaka mmoja. Kikosi kitakachovutiwa na maarifa yake kitalazimika kuweka mezani Sh6.2 bilioni ili kushawishi Barcelona kumwachilia kuondoka ugani Camp Nou.

Baada ya kuagana na Fiorentina na kutua Stamford Bridge mnamo 2016, Alonso alifunga mabao 29 kutokana na mechi 212 na kusaidia Chelsea kushinda Ligi Kuu ya Uingereza (EPL) na taji la UEFA.

Alonso ambaye babake alichezea Barcelona kati ya 1982 na 1987, alipokea malezi ya soka katika akademia ya Real kabla ya kujiunga na Bolton mnamo 2010 kisha kuhamia Fiorentina miaka mitatu baadaye.

Anakuwa beki wa tatu wa EPL kujiunga na Barcelona bila ada yoyote muhula huu baada ya Andreas Christensen na Hector Bellerin waliotokea Chelsea na Arsenal mtawalia.

TAFSIRI NA: CHRIS ADUNGO

  • Tags

You can share this post!

Auba mali ya Chelsea dakika za lala salama

Marcelo apata hifadhi mpya nchini Ugiriki baada ya...

T L