• Nairobi
  • Last Updated May 19th, 2024 9:50 AM
Bayern Munich wapepeta Inter Milan katika pambano la UEFA ugani San Siro

Bayern Munich wapepeta Inter Milan katika pambano la UEFA ugani San Siro

Na MASHIRIKA

BAYERN Munich walianza kampeni yao katika Klabu Bingwa Ulaya (UEFA) kwa ushindi wa 2-0 dhidi ya Inter Milan katika pambano la Kundi C lililowakutanisha uwanjani San Siro mnamo Jumatano usiku.

Bayern walitambishwa zaidi na fowadi wa zamani wa Manchester City, Leroy Sane, aliyefunga bao la kwanza katika dakika ya 25 kabla ya Inter kujifunga kupitia kwa beki Danilo D’Ambrosio aliyezidiwa na presha kutoka kwa Sane na Kingsley Coman.

Bayern sasa watakutana na Barcelona katika pambano la pili kundini mnamo Septemba 13, 2022. Barcelona watashuka dimbani wakilenga kulipiza kisasi na kuendeleza ubabe uliowavunia ushindi wa 5-1 dhidi ya Viktoria Plzen mnamo Jumatano usiku uwanjani Camp Nou.

Chini ya kocha Julian Naggelsman, Bayern walielekeza langoni jumla ya makombora 21 huku 11 yakilenga shabaha.

Bayern wangalifunga mabao zaidi katika kipindi cha pili ila kipa Andre Onana akajituma maradufu na kunyima fowadi Sadio Mane nafasi nyingi za wazi. Inter watakutana na Viktoria Plzen katika pambano lao lijalo mnamo Septemba 13, 2022.

TAFSIRI NA: CHRIS ADUNGO

  • Tags

You can share this post!

Kingi achaguliwa Spika wa Seneti

Lewandowski afunga mabao matatu na kusaidia Barcelona...

T L