• Nairobi
  • Last Updated May 19th, 2024 7:50 AM
Brentford wazidisha masaibu ya Burnley katika EPL

Brentford wazidisha masaibu ya Burnley katika EPL

Na MASHIRIKA

MABAO mawili mwishoni mwa kipindi cha pili kutoka kwa Ivan Toney yalivunia Brentford ushindi wa 2-0 uliodidimiza zaidi matumaini ya Burnley kukwepa shoka la kuwateremsha ngazi katika Ligi Kuu ya Uingereza (EPL) msimu huu.

Sare kwa Burnley almaarufu The Clarets ingewaondoa katika mduara wa vikosi vitatu vya mwisho jedwalini. Hata hivyo, Toney alishirikiana na Christian Eriksen katika dakika ya 85 na kufungulia Brentford ukurasa wa mabao kabla ya fowadi huyo kujaza penalti wavuni dakika tano baadaye.

Burnley walikamilisha mechi hiyo na wachezaji 10 pekee uwanjani baada ya Nathan Collins kuonyeshwa kadi nyekundu kwa hatia ya kumchezea Toney visivyo mwishoni mwa kipindi cha pili.

Huku Brentford wakishikilia sasa nafasi ya 15 kwa alama 30 jedwalini, Burnley wanakamata nambari 18 kwa pointi 21, nne pekee kuliko Norwich City wanaovuta mkia. Watford wanashikilia nafasi ya 19 kwa alama 19 kutokana na michuano 28.

Chini ya kocha Sean Dyche, Burnley kwa sasa wana ulazima wa kushinda mechi nyingi zaidi kutokana na 11 pekee ambazo zimesalia katika EPL muhula huu kuliko zile ambazo wameshinda baada ya michuano 27 ya kwanza.

Matokeo ya EPL (Jumamosi):

Brighton 0-2 Liverpool

Brentford 2-0 Burnley

Man-United 3-2 Tottenham

TAFSIRI NA: CHRIS ADUNGO

You can share this post!

Ronaldo abeba Man-United dhidi ya Tottenham ligini

Liverpool wakomoa Brighton na kuendeleza presha kwa...

T L