• Nairobi
  • Last Updated May 3rd, 2024 3:16 PM
Brighton waduwaza Liverpool kwa kuipokeza kichapo cha 3-0 katika EPL ugani Amex

Brighton waduwaza Liverpool kwa kuipokeza kichapo cha 3-0 katika EPL ugani Amex

Na MASHIRIKA

KOCHA Roberto de Zerbi amesema masogora wake wa Brighton wana kiu ya kunogesha soka ya bara Ulaya msimu ujao baada ya mabao mawili kutoka kwa Solly March na jingine kutoka kwa Danny Welbeck kuwapa ushindi wa 3-0 dhidi ya Liverpool mnamo Jumamosi ugani Amex.

March alifungulia Brighton ukurasa wa mabao baada ya kukamilisha krosi ya Kaoru Mitoma kunako dakika ya 47 kabla ya kupachika wavuni bao la pili katika dakika ya 53. Goli la pili lilikuwa zao la ushirikiano mkubwa kati yake na kiungo Alexis Mac Allister aliyemzidi maarifa beki Joel Matip mara kadhaa.

Welbeck alitokea benchi katika kipindi cha pili na kuwafungia Brighton bao la tatu dakika tisa kabla ya kipenga cha kuashiria mwisho wa mchezo kupulizwa.

“Nina kikosi kizuri cha wachezaji bora. Ni fahari tele kufanya kazi na kundi hili la wanasoka. Lengo letu kwa sasa ni kufuzu kwa soka ya bara Ulaya muhula ujao,” akasema De Zerbi.

Ilikuwa mara ya kwanza kwa Brighton almaarufu Seagulls kushinda Liverpool katika uwanja wa nyumbani wa Amex tangu Januari 14, 1961 – yapata miaka 62 iliyopita.

Brighton kwa sasa wamefunga bao katika kila mojawapo ya mechi nane zilizopita katika EPL na kujizolea jumla ya mabao 21 katika kipindi hicho.

TAFSIRI NA: CHRIS ADUNGO

  • Tags

You can share this post!

Raila aingia boksi ya Ruto

JUNGU KUU: IEBC gae Chebukati, wenzake wakistaafu

T L