• Nairobi
  • Last Updated May 2nd, 2024 10:44 AM
Chiefs yakaribisha Mkenya Teddy Akumu ikirarua Orlando Pirates gozini

Chiefs yakaribisha Mkenya Teddy Akumu ikirarua Orlando Pirates gozini

Na GEOFFREY ANENE

KAIZER Chiefs anayochezea Mkenya Anthony ‘Teddy’ Akumu ilishinda debi ya Soweto dhidi ya Orlando Pirates 1-0 na kumaliza ukame wa mechi saba bila ushindi katika mashindano ya nyumbani Jumapili.

Chiefs, ambayo ilikuwa imezoa ushindi wake wa mwisho katika mashindano ya nyumbani kwa kulemea Tshakhuma 3-0 kwenye Ligi Kuu mnamo Januari 19, ilizamisha Pirates kupitia bao la Samir Nurkovic uwanjani Soccer City.

Mshambuliaji huyo wa Serbia alipata bao hilo dakika ya 54 ya mechi hiyo ambayo Akumu alikuwa akirejea ulingoni baada ya kukosa tatu zilizopita.

Kilikuwa kisasi kitamu kwa Chiefs ambayo ilikuwa imepoteza mikononi mwa Pirates mara tatu mfululizo. Ililimwa 2-1 zilipokutana mara ya mwisho uwanjani Orlando mnamo Januari 30 katika mechi ambayo Nurkovic alipoteza penalti.

Kabla ya ushindi dhidi ya Pirates, Chiefs ya kocha Gavin Hunt ilikuwa imeshinda mchuano mmoja kati ya 11 iliyopita, dhidi ya Petro de Luanda kutoka Angola 2-0 kwenye Klabu Bingwa Ulaya mnamo Machi 6.

Ushindi huo umeinua Chiefs kutoka nafasi ya 11 hadi nambari tisa kwenye ligi hiyo ya klabu 16. Imezoa alama 23 kutokana ne mechi 19.

You can share this post!

Mbappe avunja rekodi ya ufungaji mabao katika soka ya Ligi...

Ndani ya ndoto ya wahudumu wa bodaboda wa Kangema ya kuwa...