• Nairobi
  • Last Updated May 18th, 2024 8:57 PM
Conte: Ni wakati wa Kane kuongeza kandarasi yake

Conte: Ni wakati wa Kane kuongeza kandarasi yake

IMETAYARISHWA NA CECIL ODONGO

KOCHA wa Tottenham Hot Spurs Antonio Conte amesema kuwa huu ndio wakati ambapo mshambuliaji Harry Kane anastahili kuongeza kandarasi yake na timu hiyo.

Spurs imeanza vyema msimu huu kwa kuzoa alama 10 kutoka mechi zake nne za kwanza huku Kane akifunga mabao manne kati ya tisa ambayo timu hiyo imefunga.

Nahodha huyo wa Uingereza amesalia na miaka miwili kwenye kandarasi yake na anaonekana kumakinikia kujituma kambini mwa Spurs baada ya kuvunjika moyo kwa kukosa kuhamia Manchester City wakati sawa na huu mwaka uliopita.

“Kwa hakika ningependa sana Kane atie saini kandarasi mpya. Hapa tunazungumzia mshambuliaji wa hadhi ambaye ameng’aa sana na Spurs haingependa kumwaachilia,” akasema Conte.

Kane, 29, amekuwa akilenga kushinda taji la EPL na pia mnamo Novemba na Disemba atakuwa akipigania taji la Kombe la Dunia akivalia jezi la The Three Lions.

Tangu uhamisho wa hadi Manchester City ugonge mwamba, Kane hajaonyesha dalili zozote za kurefusha kandarasi yake Spurs.

  • Tags

You can share this post!

KCB yasaini wachezaji watano zaidi kwa ajili ya Ligi Kuu

Auba mali ya Chelsea dakika za lala salama

T L