Na MASHIRIKA
MABINGWA wa Ligi Kuu ya Ukraine, Dynamo Kyiv watacheza mechi za kirafiki dhidi ya Barcelona, Paris Saint-Germain (PSG), AC Milan pamoja na vikosi vingine vya haiba kubwa barani Ulaya ili kuchangisha pesa kwa ajili ya taifa lao lililovamiwa na Urusi.
Mechi hizo za hisani zitachezewa ugenini chini ya kaulimbiu: “Mechi kwa ajili ya Amani! Tusitishe Vita!”
Ajax, Benfica na Sporting Lisbon pia wamejisajili kuwa sehemu ya vikosi vitakavyopimana nguvu na Kyiv.