• Nairobi
  • Last Updated May 12th, 2024 8:50 AM
Fahamu nani atamenyana na nani kwenye robo-fainali za Euro

Fahamu nani atamenyana na nani kwenye robo-fainali za Euro

Na MASHIRIKA

MATUMAINI ya Uingereza kutia kibindoni taji la haiba kubwa kwenye ulingo wa soka kwa mara ya kwanza tangu 1966 yalisalia hai baada ya kuwaondoa Ujerumani ambao ni mabingwa mara tatu wa Euro kwenye hatua ya 16-bora ya kipute hicho mnamo Jumanne.

Chini ya kocha Gareth Southgate, Uingereza kwa sasa watavaana na Ukraine kwenye robo-fainali itakayochezewa jijini Roma, Italia mnamo Julai 3, 2021. Ukraine iliwadengua Uswidi kwa kichapo cha 2-1 usiku wa Juni 29, 2021.

Iwapo Uingereza watafuzu kwa nusu-fainali uwanjani Wembley, basi watakutana na Jamhuri ya Czech au Denmark huku Ubelgiji, Italia au Uhispania wakiwa pazuri zaidi kukutana nao kwenye fainali.

Uhispania ya kocha Luis Enrique itavaana na Uswisi kwenye mojawapo ya mechi za robo-fainali. Uhispania waliotawazwa mabingwa wa Euro mnamo 1964, 2008 na 2012, waliwaondoa Croatia kwa kichapo cha 5-3 huku Uswisi wakibandua mabingwa wa Dunia Ufaransa kwa penalti 5-4 baada ya sare ya 3-3.

Ubelgiji watavaana na Italia kwenye gozi jingine la robo-fainali huku Jamhuri ya Czech ikipimana ubabe na Denmark.

ROBO-FAINALI ZA EURO:

Ijumaa, Julai 2:

Uswisi na Uhispania (7:00pm)

Ubelgiji na Italia (10:00pm)

Jumamosi, Julai 3:

Jamhuri ya Czech na Denmark (7:00pm)

Ukraine na Uingereza (10:00pm)

TAFSIRI NA: CHRIS ADUNGO

You can share this post!

Jinsi unavyoweza kujua una ukosefu wa protini mwilini

Wanafunzi wanane katika kituo cha kurekebisha tabia wapata...