• Nairobi
  • Last Updated May 8th, 2024 8:55 PM
Fortune yapania kusajili watatu

Fortune yapania kusajili watatu

Na JOHN KIMWERE

KOCHA wa Fortune Sacco, Nicodemus Omasete amesema wamepania kusajili wachana nyavu watatu endapo Kamati Huru inayosimamia Soka Nchini, itakubali ombi la klabu zinazoshiriki kipute cha Supa Ligi ya Taifa (NSL).

Timu za kinyang’anyiro hicho ziliomba wiki mbili za mapumziko pia licha ya kupitia matatizo ya kifedha kuruhusiwa kusajili wachezaji wapya. ”Tayari wapo wachezaji watatu tunaopania kutwaa huduma zao ambao wamekuwa wakishiriki mazoezi na wenzao tukisubiri tukubaliwe ili kukamilisha zoezi hilo,” kocha huyo alisema na kuongeza kuwa wanahitaji kujiongezea nguvu ili kujiweka pazuri kwenye juhudi za kupigania tiketi ya kupandishwa ngazi kushiriki Ligi Kuu ya Kenya (FKF-PL) muhula ujao.

Fortune Sacco ni kati ya vikosi vinavyopigana kwa udi na uvumba kuwania tiketi ya kupandishwa ngazi. Kwenye ratiba ya kipute hicho, kesho Jumamosi Fortune Sacco itakuwa katika ardhi ya nyumbani kukaribisha Silibwet FC kuwinda alama tatu muhimu ili kujiongezea tumaini la kuibuka kati ya nafasi mbili na kuvuna tiketi ya kusonga mbele.

Hata hivyo mechi hizo zinashuhudia ushindani mkali ambapo Shabana FC inafuata Fortune sako kwa bako. Shabana leo itacheza dhidi ya Murang’a Seal ambapo ikishinda itaibandua Fortune Sacco katika nafasi ya pili.

Kwenye jedwali, Maafande wa APs Bomet wanaongoza kwa alama 37, tatu mbele ya Fortune Sacco. Shabana inafunga tatu bora kwa alama 31, moja mbele ya Zoo Kericho

You can share this post!

Ushindani mkali kushuhudiwa mechi za KWPL

Miamba wabwagwa mchujoni

T L