Na MASHIRIKA
KIUNGO mzoefu wa Arsenal, Matteo Guendouzi, 23, ameingia katika sajili rasmi ya Olympique Marseille kwa kima cha Sh1.3 bilioni baada ya kuridhisha vinara wa kikosi hicho cha Ligi Kuu ya Ufaransa (Ligue 1) kilichomsajili kwa mkopo mnamo 2020-21.
Guendouzi alichezea Marseille mara 55 mnamo 2020-21 na akapata fursa ya kuwajibishwa katika timu ya taifa ya Ufaransa.
Guendouzi alisakatia Arsenal katika mechi 82 na akawachezea mara ya mwisho mnamo Juni 2020. Kiungo huyo anasajiliwa na Marseille kwa mkataba wa kudumu siku ambapo kocha Jorge Sampaoli aliagana rasmi na kikosi hicho.
TAFSIRI NA: CHRIS ADUNGO