• Nairobi
  • Last Updated May 18th, 2024 8:57 PM
GUMZO LA SPOTI: Mtangoja sana, Viera aambia Arsenal na Chelsea wanaommezea Wilfried Zaha

GUMZO LA SPOTI: Mtangoja sana, Viera aambia Arsenal na Chelsea wanaommezea Wilfried Zaha

IMETAYARISHWA NA CECIL ODONGO

KOCHA wa Crystal Palace Patrick Viera amesisitiza kuwa nyota wake Wilfried Zaha hatahamia Chelsea au Arsenal hivi karibuni kwa kuwa lengo lake ni kutambisha timu hiyo kutwaa mataji mengi.

Kulikuwa na ripoti kuwa Zaha alikuwa tayari kubanduka Selhurst Park na kuelekea Chelsea au Arsenal lakini uhamisho huo haukufanyika kabla ya makataa ya mnamo Alhamisi.

“Zaha anamakinikia kusalia hapa timuni na lengo lake ni kushinda mataji. Jinsi ninavyoona anavyojituma, ni wazi kuwa nia yake si kuhamia timu yoyote bali kuitumikia Crystal Palace,” akasema Viera, mchezaji wa zamani wa Arsenal.

Zaha, 29, raia wa Ivory Coast ameshaanza kuwa moto wa kuotea mbali sana msimu huu huku akifunga mabao matatu katika mechi tatu alizowajibikia waajiri wake.

Arsenal ilikuwa ikiwinda Zaha baada ya kumkosa 2019 lakini juhudi zao zilikosa kuzaa matunda kwa mara nyingine.

  • Tags

You can share this post!

VITUKO: Penzi la Balotelli na Messina laingia doa akirudia...

KCB yasaini wachezaji watano zaidi kwa ajili ya Ligi Kuu

T L