• Nairobi
  • Last Updated May 18th, 2024 8:57 PM
VITUKO: Penzi la Balotelli na Messina laingia doa akirudia kichuna wa awali

VITUKO: Penzi la Balotelli na Messina laingia doa akirudia kichuna wa awali

IMETAYARISHWA NA CHRIS ADUNGO

UHUSIANO kati ya kipusa Alessia Messina, 29, na mfumaji wa zamani wa Manchester City na Liverpool, Mario Balotelli sasa umeingiwa na mdudu.

Hii ni baada ya Balotelli, 32, kuanza kuwasha upya mwenge wa mapenzi na mchumba wake wa zamani, Clelia – mwanabenki na mwanamitindo maarufu nchini Uswisi aliyemburudisha kwa miezi sita kabla ya kutemana naye mnamo 2019.

Wawili hao walionekana wakiponda raha jijini Zurich wiki hii baada ya kuripotiwa kuwa Clelia alikuwa akimsukuma Balotelli kujiunga na FC Sion inayoshiriki Ligi Kuu ya Uswisi.

Awali, Balotelli ambaye pia ni raia wa Italia, alikuwa amewataka mashabiki wake kujiandaa kwa sherehe kubwa ya ndovu kumla mwanawe mwishoni mwa mwaka huu 2022 kwa kuwa alipanga kufunga pingu za maisha na Messina mnamo Disemba 2022.

Mpambe aliyetarajiwa kusimamia harusi hiyo ni kiungo matata wa Juventus na timu ya taifa ya Ufaransa, Paul Pogba ambaye kwa sasa anatoka kimapenzi na kipusa Maria Zulay Salaues.

Balotelli alimvisha Messina pete ya uchumba mnamo Septemba 2020 baada ya kufahamiana kwa kipindi cha mwezi mmoja pekee.

Messina ambaye alikuwa mwaniaji wa taji la uanamitindo katika mashindano ya Big Brother, Temptation Island na Grande Fratello mnamo 2019, anajivunia zaidi ya wafuasi laki nane kwenye mitandao ya kijamii.

  • Tags

You can share this post!

NYOTA WA WIKI: Gabriel Jesus

GUMZO LA SPOTI: Mtangoja sana, Viera aambia Arsenal na...

T L