• Nairobi
  • Last Updated May 19th, 2024 10:50 AM
Hoki: Vipusa wa kitaifa waanza Jamhuri Cup kwa madaha

Hoki: Vipusa wa kitaifa waanza Jamhuri Cup kwa madaha

Na ABDULRAHMAN SHERIFF

TIMU ya taifa ya hoki ya wanawake (KWXV) jana ilianza vyema mashindano ya mchezo wa hoki ya Jamhuri Cup, ikishinda mechi zake mbili za mwanzo katika uwanja wa Mombasa Sports Club.

Timu hiyo ya KWXV ilianza kampeni yao kwa kuitandika wasichana wa nyumbani Mombasa Sports Club (MSC) Ladies kwa mabao 2-0. Mabao hayo yalifungwa na Aurelia Atieno kwenye dakika ya nane na Maureen Okumu kunako dakika ya 22.

Katika mechi yao ya pili, wachezaji hao wa KWXV walifanikiwa kuichapa timu ya The Swan kwa mabao 3-0. Mabao ya washindi yalifungwa na Rhoda Auira dakika ya saba, Aurelia Atieno dakika ya 28 na Gilly Okumu dakika ya 29. Katika mechi hiyo, Aurelia alifunga bao lake la pili katika mashindano hayo.

Lakini timu ya taifa ya wanaume ilianza vibaya baada ya kutandikwa bao 1-0 na Underdogs. Bao la ushindi la Underdogns lilipatikana kwenye dakika ya 17 na Timothy Juma aliyeingia dakika ya tisa.Timu ya Kenya Police ambayo ni mlojawapo ya zile zinazopigiwa upatu wa kushinda mashindano hayo, ilifanikiwa kuifunga Mombasa West yenye wanafunzi kadhaa wa shule St Charles Lwanga ya Changamwe kwa mabao 2-0.Brian Saina na Govan Mbeki ndio waliofunga mabao ya Police kwenye dakika ya tatu na 21.

Nayo Parkroad ilifanikiwa kupata ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Tuskforce ilhali Green Sharks na Mvita XV zilitoshana nguvu kwa kutoka sare ya kutofungana.Western Jaguars kutoka Kakamega iliweza kupata ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya timu ya wanaume ya Mombasa Sports Club.

Nao Amira Sailors wakahiari kichapo cha mabao matatu bila jibu kutoka kwa Blazers.Mashindano hayo yanadhaminiwa na kampuni ya Daikyo Japan Motors ambayo pia ina kikosi chake katika kombe hilo.

You can share this post!

Mbivu na mbichi kujulikana leo duru ya Guru Nanak Rally...

6 waotea kiti cha Ojaamong

T L