Na MASHIRIKA
MATUMAINI ya Juventus kufuzu kwa soka ya Klabu Bingwa Ulaya (UEFA) msimu ujao wa 2022-23 yalididimizwa na Bologna waliowalazimishia sare ya 1-1 mnamo Jumamosi usiku ugani Allianz Stadium.
Marko Arnautovic aliyepachika wavuni bao lake la 11 katika Ligi Kuu ya Italia (Serie A) msimu huu aliwaweka Bologna kifua mbele katika dakika ya 52.
Hata hivyo, Juventus walirejea mchezoni Bologna waliposalia na wachezaji tisa pekee uwanjani baada ya Adama Soumaoro na Gary Medel kuonyeshwa kadi nyekundu katika dakika ya 84.
Dusan Vlahovic alisawazishia Juventus katika dakika ya 90 na kunyima Bologna ushindi. Juventus kwa sasa wanashikilia nafasi ya nne kwenye msimamo wa jedwali la Serie A kwa alama 63, sita zaidi kuliko AS Roma watakaovaana na Napoli mnamo Aprili 18, 2022. Bologna walisalia katika nafasi ya 13 kwa pointi 38.
MATOKEO YA SERIE A (Jumamosi):
Juventus 1-1 Bologna
Cagliari 1-0 Sassuolo
Sampdoria 1-2 Salernitana
Udinese 4-1 Empoli
Fiorentina 1-0 Venezia
Lazio 1-1 Torino
TAFSIRI NA: CHRIS ADUNGO