• Nairobi
  • Last Updated May 18th, 2024 7:05 PM
Juventus waingia ndani ya 10-bora jedwalini baada ya kushinda mechi ya pili mfululizo Serie A

Juventus waingia ndani ya 10-bora jedwalini baada ya kushinda mechi ya pili mfululizo Serie A

Na MASHIRIKA

JUVENTUS walipaa hadi ndani ya orodha ya 10-bora kwenye msimamo wa jedwali la Ligi Kuu ya Italia (Serie A) baada ya kuwapepeta Sampdoria 3-2 na hivyo kusajili ushindi wa pili mfululizo ligini muhula huu.

Paulo Dybala aliwafungulia Juventus ukurasa wa mabao katika dakika ya 10 ila akaondoka uwanjani kwa machozi tele baada ya kupata jeraha baya sekunde chache baadaye.

Ingawa Leonardo Bonucci alifungia Juventus bao la pili kupitia penalti, Maya Yoshida alifanya mambo kuwa 2-1 kabla ya kipenga cha kuashiria mwisho wa kipindi cha kwanza kupulizwa.

Manuel Locatelli alizamisha kabisa chombo cha Sampdoria waliojitahidi kurejea mchezoni kupitia Antonio Candreva.Kabla ya kubwaga Sampdoria, mchuano wa mwisho kwa Juventus kushinda katika Serie A muhula huu ulikuwa dhidi ya Spezia waliopokezwa kichapo cha 3-2

Alama mbili kutokana na mechi nne za ufunguzi wa msimu huu zilikuwa zimesaza Juventus ya kocha Massimiliano Allegri ndani ya orodha ya vikosi vitatu vya mwisho jedwalini.

  • Tags

You can share this post!

Bruno Fernandes asema hataachia Ronaldo jukumu la kuchanja...

Fati arejea kikosini na kuwabeba Barcelona dhidi ya Levante...