• Nairobi
  • Last Updated May 18th, 2024 8:57 PM
Kerich akamata nafasi ya pili Doha Marathon, Kipchirchir na Cheptoo nambari tatu

Kerich akamata nafasi ya pili Doha Marathon, Kipchirchir na Cheptoo nambari tatu

Na GEOFFREY ANENE

WAKENYA Gevin Kerich na Victor Kipchirchir wameridhika na nafasi ya pili na tatu mtawalia nyuma ya Mmoroko Mohcin Outalha kwenye mashindano ya Ooredoo Doha Marathon nchini Qatar, Ijumaa.

Outalha amekata utepe katika mbio hizo za kilomita 42 kwa saa 2:06:49, sekunde tatu mbele ya Kerich (2:06:52) naye Kipchirchir akafunga tatu-bora kwa 2:06:54.

Muethiopia Adane Kebede amefuata katika nafasi ya nne kwa 2:06:54 huku Mkenya Zablon Chumba akiwa wa tano (2:07:13). Wakenya wengine katika 10-bora ni Thomas Kiplagat (2:16:48) na Bernard Ng’eno (2:17:49) katika nafasi ya tisa na kumi mtawalia.

Mkenya wa kwanza katika kitengo cha kinadada ni Beatrice Cheptoo katika nafasi ya tatu kwa saa 2:22:28. Muethiopia Meseret Belete (2:20:46) na Mbahraini Desi Mokonin (2:20:47) wamefagia nafasi mbili za kwanza mtawalia. Wakenya Emily Arusio (2:25:22), Makala haya ya 11 yalivutia washiriki 8,000.

Wakati huo huo, Mkenya Ruben Kiprop Kipyego ameingia mbio za Zurich Maratón de Sevilla nchini Uhispania zitakazofanyika Februari 19. Kipyego anajivunia muda bora wa saa 2:03:55.

  • Tags

You can share this post!

Man-United na Palace watoshana nguvu kwa sare ya 1-1 katika...

Namwamba apongeza majagina kwa kujitolea kuimarisha vipaji...

T L