• Nairobi
  • Last Updated May 18th, 2024 10:55 AM
Kimathi atua Ulaya kutafuta pointi Rally Estonia

Kimathi atua Ulaya kutafuta pointi Rally Estonia

Na GEOFFREY ANENE

DEREVA McRae Kimathi anatumai mambo yatamwendea vyema kwenye duru ya nne ya Mbio za Magari za Dunia za Chipukizi (JWRC) nchini Estonia mnamo Julai 14-17.

Bingwa huyo wa Afrika kitengo cha chipukizi mwaka 2021 alisafiri hadi Estonia mnamo Alhamisi. Alieleza Taifa Leo kuwa yeye na mwelekezi wake Mwangi Kioni walikosa bahati kwenye duru ya Mbio za Magari Duniani (WRC) ya Safari Rally iliyofanyika Nairobi na Naivasha mwezi Juni.

“Hata hivyo, akili zetu zote sasa ziko Estonia. Kujaribu kupata ujuzi na kukamilisha mbio hizo,” alisema Kimathi aliyekamata nafasi ya 23 kati ya madereva 42 walioshiriki Safari Rally na kumaliza nambari tatu katika kitengo cha chipukizi nyuma ya mwanadada Maxine Wahome na Jeremiah Wahome. Maxine, Jeremiah na Hamza Anwar pia wanatarajiwa kuwa Estonia kupokea mafunzo baada ya kudhaminiwa na Safaricom na Kenya Airways.

Wote wanne wanapaisha magari ya Ford Fiesta R3. Aidha, mashindano ya Sunset Corsa yanayoendeshwa na Daimlar Motorsports Kenya yatafanyika wikendi hii katika maeneo ya Masinga.

  • Tags

You can share this post!

TAHARIRI: Vituko vya Nick, serikali vyatamausha Starlets...

West Ham wajinasia maarifa ya beki Flynn Downes kutoka...

T L