• Nairobi
  • Last Updated May 18th, 2024 7:55 AM
West Ham wajinasia maarifa ya beki Flynn Downes kutoka Swansea City

West Ham wajinasia maarifa ya beki Flynn Downes kutoka Swansea City

Na MASHIRIKA

WEST Ham United wamejinasia huduma za kiungo mahiri wa Swansea City, Flynn Downes, 23, kwa mkataba wa miaka mitano uliogharimu Sh1.8 bilioni.

Downes aliingia katika sajili ya Swansea mwishoni mwa msimu wa 2020-21 kwa mkataba wa miaka minne. Alitia fora kambini mwa kikosi hicho kiasi cha kuwa kivutio cha klabu nyingi za bara Ulaya.

Sasa atavalia jezi nambari 12 mgongoni katika uwanja wa London Stadium kambini mwa West Ham wanaotiwa makali na kocha David Moyes.

Chipukizi huyo wa zamani wa Uingereza U-20 alizaliwa katika eneo la Brentwood, Essex, na akawajibishwa katika kikosi cha kwanza cha Ipswich mnamo 2017 huku akivalia jezi za kikosi hicho mara 99 katika mashindano yote.

Alichezeshwa na Swansea mara 32 katika Ligi ya Daraja ya Kwanza nchini Uingereza (Championship) na kusaidia kikosi hicho kuambulia nafasi ya 15 jedwalini.

TAFSIRI NA: CHRIS ADUNGO

You can share this post!

Kimathi atua Ulaya kutafuta pointi Rally Estonia

MITAMBO: Mashine ya kisasa inayosaga nyasi za mifugo na...

T L