• Nairobi
  • Last Updated May 18th, 2024 7:05 PM
Kipusa Mbuche kusajiliwa na TSC Queens ya Tanzania

Kipusa Mbuche kusajiliwa na TSC Queens ya Tanzania

Na ABDULRAHMAN SHERIFF

Mwanasoka wa Fortune Ladies FC, Mbuche Said anatarajiwa kurudi Tanzania na kusajiliwa tena na klabu ya Ligi Kuu ya Soka ya Wanawake ya TSC Queens FC ya mjini Mwanza.

Akiongea na ‘Taifa Leo’ baada ya kuichezea timu yake ya nyumbani Waa ya Swabrina Queens FC kwenye mashindano ya Rashid Abdalla Super Cup, Mbuche amesema klabu hiyo ya TSC Queens inafanya mipango ya kutaka kumsajili tena kwa msimu huu.

Akiwa na umri wa miaka 24 na hapo awali kuwahi kuzichezea klabu za Mombasa Olympic Ladies na Ukunda Queens FC, Mbuche amesema ana nia kubwa ya kufanya vizuri katika klabu hiyo ya Mwanza.“Nina hamu kubwa ya kuendeleza kipawa cha uchezaji wangu nikiwa na nia ya kutaka kucheza soka la kulipwa huko barani Ulaya.

Nina imani kwa kucheza ligi ya Tanzania, ni wepesi zaidi kuonekana kwani mara kwa mara huwa zinaangaziwa kwenye televisheni na vyombo vya habari za huko,” akasema.Mbuche anasema ana imani kubwa baada ya msimu huu, anatarajia na kwa uwezo wa Mungu, ana tamaa ya kwenda ng’ambo kuchezea timu yoyote huko.

“Nina hamu ya kucheza soka la kulipwa huko ng’ambo kwani ukifika huko ndiko kwenye kuthaminiwa soka letu,” akasema.?Kwa wakati huu, Mbuche anayechezea safu ya sentahafu ni mchezaji wa klabu ya Fortune Ladies FC ambayo inaongoza kwenye Ligi ya FKF ya Kaunti ya Mombasa.

You can share this post!

Wakenya 4 waona giza tenisi ya Afrika ya Under-18 ikianza...

Wanyama aongoza klabu kutwaa ubingwa Canada

T L