• Nairobi
  • Last Updated May 19th, 2024 9:01 PM
KWPL: Kangemi, Kayole na Bunyore zaangukiwa na shoka

KWPL: Kangemi, Kayole na Bunyore zaangukiwa na shoka

Na JOHN KIMWERE

KANGEMI Starlets, Kayole Starlets na Bunyore Starlets kila moja imeshushwa daraja kutoka Ligi Kuu ya Soka la Kenya (KWPL) baada ya kumaliza za tatu mwisho kwenye msimamo wa jedwali baada ya kukamilika msimu wa kipute hicho muhula huu.

Nayo Vihiga Queens imevishwa taji la ngarambe ya msimu huu ambapo kwenye mechi ya mwisho ilinyuka Bunyore Starlets mabao 2-1.

Topister Situma alifunga mabao hayo na kutwaa tuzo ya mfungaji bora muhula huu kwa kutikisa wavu mara 17.

Naye Fasila Adhiambo wa Kangemi Starlets ilimaliza wa pili kwa kucheka na wavu mra 14. Warembo hao waliomaliza kwa alama 60 kwa kushinda mechi 19 na kutoka nguvu sawa mara tatu pia ilipongezwa kwa Sh1 milioni.

”Ninashukuru wachezaji wangu kwa kutimiza azma yetu kubeba taji tena bila kupoteza mechi yoyote,” kocha wa Vihiga Queens, Boniface Nyamunyamu alisema na kuongeza hakuna kupumua kwa kuwa tayari wameanza kuwazia kampeni za msimu ujao.

Kwenye mechi za kutamatisha kipute hicho, Ulinzi Starlets ilitoka nguvu sawa mabao 3-3 dhidi ya Zetech Sparks na kumaliza ya pili kwa alama 43.

Gaspo Women ilizaba Trans Nzoia Falcons mabao 2-0, Kangemi iling’atwa mabao 2-0 na Nakuru City Queens nayo Wadadia ilitoka bao 1-1 na Thilka Queens.

  • Tags

You can share this post!

Wapinzani wa Nassir walia serikali ya Joho inawatesa

Uswisi waduwaza Ureno katika Uefa Nations League

T L