• Nairobi
  • Last Updated May 19th, 2024 9:01 PM
Uswisi waduwaza Ureno katika Uefa Nations League

Uswisi waduwaza Ureno katika Uefa Nations League

Na MASHIRIKA

HARIS Seferovic alifunga bao la haraka zaidi kwenye historia fupi ya kipute cha Uefa Nations League katika ushindi wa 1-0 uliosajiliwa na Uswisi dhidi ya Ureno katika Kundi la A2 mnamo Jumapili usiku jijini Geneva.

Fowadi huyo wa Benfica aliwaweka Uswisi kifua mbele baada ya sekunde 55 za kipindi cha kwanza. Ingawa Seferovic alitatiza tena mabeki wa Ureno katika kipindi cha pili, Ureno walitamalaki mchezo na kumwajibisha vilivyo kipa Jonas Omlin.

Omlin alipangua makombora mazito aliyoelekezewa na Danilo Pereira, Goncalo Guedes na Bernardo Silva walioshirikiana vilivyo na Joao Cancelo na Diogo Jota. Ureno waliotawazwa mabingwa wa Nations League mnamo 2019, walimpumzisha nyota Cristiano Ronaldo katika pambano hilo dhidi ya Uswisi.

Kichapo hicho kiliwateremsha hadi nafasi ya pili kwenye msimamo wa Kundi A2 baada ya Uhispania kupepeta Jamhuri ya Czech 2-0.

TAFSIRI NA: CHRIS ADUNGO

  • Tags

You can share this post!

KWPL: Kangemi, Kayole na Bunyore zaangukiwa na shoka

Uhasama wa ndani watesa miungano

T L