• Nairobi
  • Last Updated May 19th, 2024 10:50 AM
KWPL: Vita vya Gaspo Women na Vihiga Queens kutwaa ubingwa vyafika patamu

KWPL: Vita vya Gaspo Women na Vihiga Queens kutwaa ubingwa vyafika patamu

NA AREGE RUTH

RAUNDI ya 18 ya mechi za Ligi Kuu ya Wanawake nchini (KWPL) itachezwa wikendi hii.

Gaspo Women na Vihiga Queens zinapambania kutwaa ubingwa huku vita vya kukwepa kushushwa daraja vikipamba moto.

Vinara wa ligi Gaspo wana alama 40 sawa na Vihiga lakini wanatofautiana na mabao matatu.

Gaspo wanahitaji pointi tatu kusalia kileleni mwa jedwali watakapokabiliana na Kisumu All Starlets katika uwanja wa GEMS Cambridge kesho Jumamosi.

Katika mechi zao tano wakiwa nyumbani, Gaspo imeshinda mechi zote ikiwemo ushindi wa mabao 3-1 dhidi ya Bunyore Starlets wikendi iliyopita.

Ugani Moi mjini Kisumu, Thika Queens watatafuta mbinu ya kulipiza kisasi dhidi ya Vihiga Queens baada ya kipigo cha 4-1 dhidi ya Wadadia Women wikendi iliyopita.

Katika uwanja wa Mumias Sports Complex ulioko Kaunti ya Kakamega, Wadadia walio nafasi ya nne wanatarajia kuendeleza msururu wao matokeo mazuri watakapo kabana koo na Ulinzi Starlets.

Trans Nzoia Falcons watagaragazana na Kayole Starlets ambao mkiani kwenye jedwali katika uwanja wa Ndura Sports Complex mjini Kitale Jumapili.

Kwa upande mwingine, Kangemi Ladies itasafiri hadi Magharibi mwa Kenya kutoana kijasho na Bunyore Starlets katika uwanja wa Mumboha Grounds, Luanda kaunti ya Vihiga huku Zetech Sparks ikicheza na Nakuru City Queens ugani Cambridge.

  • Tags

You can share this post!

DPP aagizwa awape ushahidi washukiwa wa ulaghai wa dhahabu

Aliyejifanya Kenyatta na kutapeli bwanyenye Sh10 milioni...

T L