• Nairobi
  • Last Updated May 1st, 2024 1:33 PM
Lautaro Martinez asaidia Inter kuangusha AC Milan katika gozi la Serie A ugani San Siro

Lautaro Martinez asaidia Inter kuangusha AC Milan katika gozi la Serie A ugani San Siro

Na MASHIRIKA

LAUTARO Martinez alifunga bao la pekee lililovunia Inter Milan ushindi wa 1-0 dhidi ya watani wao wakuu AC Milan katika Ligi Kuu ya Italia (Serie A) ugani San Siro mnamo Jumapili.

Matokeo hayo yalidumisha Inter katika nafasi ya pili kwenye msimamo wa jedwali kwa alama 13 nyuma ya viongozi Napoli wanaoselelea kileleni kwa pointi 56 baada ya kutandika Spezia 3-0.

Nahodha wa Inter, Martinez, alifunga bao lake kwa kichwa kutokana mpira wa kona uliopigwa na kiungo wa zamani wa Milan, Hakan Calhanoglu.

Mabao mawili ya Inter yalikataliwa mwishoni mwa kipindi cha pili baada ya kubainika kwamba Romelu Lukaku alifunga baada ya kumchezea Malick Thiaw visivyo naye Martinez alicheka tena na nyavu za wapinzani wao akiwa ameotea.

Matokeo hayo yalishuhudia Milan wakiteremka hadi nafasi ya sita jedwalini kwa alama 38 sawa na Atalanta na Lazio wanaofunga mduara wa nne-bora. Milan sasa wamepoteza mechi tano kati ya sita zilizopita katika mashindano yote.

Chini ya kocha Stefano Pioli, mabingwa hao watetezi wa Serie A hawakueleza kombora lolote langoni mwa Inter hadi dakika ya 75 ambapo kipa Andre Onana wa Inter alipowajibishwa vilivyo na Brahim Diaz.

Ushindi wa Napoli uliwaweka pazuri kunyanyua ufalme wa Serie A msimu huu baada ya mabao yao dhidi ya Spezia kujazwa kimiani na fowadi Khvicha Kvaratskhelia wa Georgia na mvamizi matata raia wa Nigeria, Victor Osimhen aliyefunga mawili.

MATOKEO YA SERIE A (Jumapili):

Inter Milan 1-0 AC Milan

Spezia 0-3 Napoli

Torino 1-0 Udinese

Fiorentina 1-2 Bologna

TAFSIRI NA: CHRIS ADUNGO

  • Tags

You can share this post!

MWALIMU WA WIKI: Kirika atamba si darasani si ugani

Murang’a Seal yashinda na kujiongezea matumaini ya...

T L