• Nairobi
  • Last Updated May 1st, 2024 7:53 AM
Murang’a Seal yashinda na kujiongezea matumaini ya kufuzu

Murang’a Seal yashinda na kujiongezea matumaini ya kufuzu

NA JOHN ASHIHUNDU

USHINDI wa 3-0 dhidi ya Mara Sugar katika pambano la Supa Ligi (NSL) umeongeza matumaini ya Murang’a Seal FC kufuzu kwa Ligi Kuu ya Kenya (FKF-PL) msimu ujao.

Vijana hao chini ya kocha Ezekiel Akwana wamepanda hadi nafasi ya pili jedwalini, mbele ya Kibera Black Stars ambao wamekuwa wakiimiliki nafasi hiyo kwa wiki kadhaa.

Nafasi ya kwanza itashikiliwa na Shabana FC ambao wanaoongoza kwa pointi 25, mbele ya Murang’a walio na 18, wakati Black Stars wakifuata kwa pointi 17. Gusii FC ni ya nne kwa pointi 14, mbele ya Mara Sugar walio na 14.

Kutokana na mwenendo mzuri katika mechi zao tangu msimu uanze, kocha Akwana amewashauri vijana wake wajitahidi kuhakikisha wanaendelea kupata matokeo mazuri katika miaka ijayo, licha ya upinzani mkali kutoka kwa Shabana na Black Stars.

Licha ya kutopangiwa mechi mwishoni mwa wiki, Shabana wanaendelea kuongoza kwa mwanya wa poiinti saba mbele ya Murang’a Seal ambao kesho watakuwa mjini Wundanyi kucheza na Mwatate United.

Shabana maarufu kama The Glamour Boys wakuwa na ziara Nairobi kukabiliana na Kibera Black Stars at ugani Ligi Ndogo.

Mechi nyingine inayotarajiwa kuvutia mashabiki wengi itakuwa kati ya Coastal Heroes na Migori Youth katika uwanja wa Mbaraki Sports Club, wakati Vihiga United wakiisubiri Darajani Gogo mjini Mumias katika mechi nyingine ya katikati mwa wiki.

Darajani wanarejea uwanjani baada ya kuagana 0-0 na Naivas kwenye mechi iliyochezewa Hope Centre in Kawangware, Jumamosi.

Licha ya sare hiyo ya kutofungana, kocha Caleb Aringa amesisitiza kwamba matumaini yao ya kufuzu kwa ligi kuu msimu ujao yangalipo.

Matokeo ya mechi za wikendi yalikuwa: Murang’a Seal 3 Mara Sugar 0, Darajani Gogo 0 Naivas 0, Silibwet Leon 0 SS Assad 0, MCF 2 Mwatate United 2, Gusii United 1 Coastal Heroes 0, Kajiado FC 0 Mombasa Elite 1.

# Timu P W D L F A GD Pointi
1 Shabana 9 8 1 0 15 2 13 25
2 Murang’a Seal 8 5 3 0 14 5 9 18
3 Kibera Black Stars 8 5 5 1 13 3 10 17
4 Gusii 7 4 2 1 19 7 12 14
5 Mara Sugar 9 4 2 3 5 6 -1 14
6 Kisumu Allstars 8 3 4 1 12 7 5 13
7 Migori Youth 8 3 4 1 6 3 3 13
8 Naivas 8 3 3 2 10 4 6 12
9 Darajani Gogo 8 3 3 2 8 5 3 12
10 Coastal Heroes 9 3 1 5 9 13 -4 10
11 MCF 9 1 6 2 6 5 1 9
12 Mombasa Elite 9 1 4 4 6 10 -4 7
13 Kajiado 7 1 1 5 10 15 -5 4
14 Silibwet 9 1 4 4 3 12 -9 4
15 SS Assad 9 3 1 5 2 12 -10 4
16 Vihiga United 8 0 3 5 3 21 -18 0
17 Mwatate United 9 1 2 6 1 20 -19 -1
18 Fortune Sacco 3 0 0 3 -6 6 -12 -9
19 APS Bomet 0 0 0 0 0 0 0 0
  • Tags

You can share this post!

Lautaro Martinez asaidia Inter kuangusha AC Milan katika...

KWPL: Mvua ya mabao kwenye raundi ya nane

T L