• Nairobi
  • Last Updated April 28th, 2024 3:07 PM
Liverpool wakomoa Newcastle na kuweka hai matumaini ya kumaliza msimu na mataji manne

Liverpool wakomoa Newcastle na kuweka hai matumaini ya kumaliza msimu na mataji manne

Na MASHIRIKA

LIVERPOOL waliweka hai matumaini ya kujizolea jumla ya mataji manne katika kampeni za msimu huu baada ya kupokeza Newcastle United kichapo cha 1-0 katika Ligi Kuu ya Uingereza (EPL) ugani St James’ Park.

Bao la pekee na la ushindi katika mchuano huo lilipachikwa wavuni na kiungo raia wa Guinea, Naby Keita katika dakika ya 19.

Kocha Jurgen Klopp alikifanyia kikosi chake cha Liverpool mabadiliko matano yaliyoshuhudia nyota Mohamed Salah ambaye ni mfungaji bora wa EPL kufikia sasa akipangwa benchi. Liverpool ambao tayari wametawazwa mabingwa wa Carabao Cup, sasa wanajivunia alama 82 kutokana na mechi 34 za EPL huku Newcastle wakiwa na pointi 43.

Baada ya kurudiana na Villarreal kwenye nusu-fainali ya Klabu Bingwa Ulaya (UEFA) mnamo Jumanne, Liverpool wataalika Tottenham Hotspur kisha kuendea Aston Villa ligini kabla ya kukwaruzana na Chelsea kwenye fainali ya Kombe la FA mnamo Mei 14 ugani Wembley. Watafunga msimu kwa michuano miwili ya EPL dhidi ya Southampton na Wolves mtawalia.

Sadio Mane na Diogo Jota wangalifunga mabao zaidi kwa upande wa Liverpool ila wakazidiwa ujanja na kipa Martin Dubravka.

TAFSIRI NA: CHRIS ADUNGO

  • Tags

You can share this post!

Wakala wa soka, Mino Raiola, aaga dunia akiwa na umri wa...

Familia ya hayati yammiminia sifa kwa malezi bora

T L