• Nairobi
  • Last Updated May 10th, 2024 7:55 PM
Liverpool yapiga Southampton na kulazimisha mshindi wa EPL msimu huu kupatikana siku ya mwisho ya kampeni

Liverpool yapiga Southampton na kulazimisha mshindi wa EPL msimu huu kupatikana siku ya mwisho ya kampeni

Na CHRIS ADUNGO

MSHINDI wa Ligi Kuu ya Uingereza (EPL) msimu sasa atajulikana siku ya mwisho ya kampeni baada ya Liverpool kutoka nyuma na kupokeza Southampton kichapo cha 2-1 mnamo Mei 17, 2022 ugani St Mary’s.

Liverpool walishuka dimbani wakiwa na ulazima wa kushinda ili kuendeleza presha kwa viongozi na mabingwa watetezi wa EPL, Manchester City.

Kufikia sasa, Liverpool wanashikilia nafasi ya pili jedwalini kwa alama 89 huku Man-City wakijivunia pointi 90 baada ya kutandaza pia jumla ya mechi 37.

Nathan Redmond aliwaweka Southampton kifua mbele kunako dakika ya 13 kabla ya Liverpool kurejea mchezoni kupitia kwa Takumi Minamino kisha Joel Matip akapachika wavuni goli la ushindi katika dakika ya 67.

Liverpool walikifanyia kikosi chao kilichocheza dhidi ya Southampton mabadiliko tisa siku chache baada ya kupepeta Chelsea kwa penalti 6-5 na kutia kapuni ubingwa wa Kombe la FA.

Man-City watahifadhi taji la EPL msimu huu iwapo watakomoa Aston Villa ugani Etihad mnamo Mei 22.

Kukosekana kwa Mohamed Salah, Sadio Mane na Luis Diaz aliyetiwa benchi kulimweka fowadi Roberto Firmino katika ulazima wa kuongoza safu ya mbele ya Liverpool.

TAFSIRI NA: CHRIS ADUNGO

  • Tags

You can share this post!

RIWAYA: Umuhimu wa Ridhaa kukuza maudhui na kuendeleza ploti

Hofu ya baa la njaa viwavijeshi wakivamia mimea katika...

T L