NA MASHIRIKA
MANCHESTER City wameafikiana na Leeds United kumsajili kiungo wa Uingereza, Kalvin Phillips kwa Sh6.6 bilioni ili kujaza pengo la kigogo Fernandinho Luiz Roza atakayeondoka Etihad mwezi huu Juni 2022 baada ya kuhudumu ugani Etihad kwa kipindi cha miaka tisa.
Phillips, 26, amechezea Leeds mara 214 tangu aanze kuvalia jezi za kikosi cha kwanza mnamo 2015.
Sasa anakabiliwa na ushindani mkali kutoka kwa Jude Bellingham, Jordan Henderson, Conor Gallagher na James Ward-Prowse ili kuwa sehemu ya kikosi kitakachotegemewa na Uingereza katika fainali za Kombe la Dunia za 2022 nchini Qatar.
TAFSIRI NA: CHRIS ADUNGO