• Nairobi
  • Last Updated May 19th, 2024 9:50 AM
Mat Ryan hatua moja kutua Real Sociedad

Mat Ryan hatua moja kutua Real Sociedad

Na MASHIRIKA

MLINDA-LANGO wa Brighton Mat Ryan yuko tayari kujiunga na Real Sociedad ya Uhispania kwa malipo ambayo hayafichuliwa.

Ryan, 29, anatarajiwa kufanyiwa vipimo vya kimatibabu wiki hii kabla ya kujiunga na klabu hiyo, baada ya makubaliano ya kibinafsi kukamilika.

Timu kadhaa za Uhispania na timu ya Arsenal zilipendezwa na mchezaji huyo ambaye yuko mwaka wake wa mwisho wa mkataba na timu ya Brighton. Alijiunga na Arsenal kwa mkopo Januari na kucheza jumla ya mechi tatu.

Kocha wa Celtic ya Scotland, Ange Postecoglou pia alitaka kumhusisha katika kikosi chake, baada ya mafanikio yao katika timu ya taifa ya Australia.

Ryan alikuwa nambari moja katika kikosi katika kikosi cha Postecoglou kilichoshiriki Kombe la Dunia 2014, na pia kikosi kilichoibuka mabingwa wa Klabu Bingwa bara la Asia 2015.

kuwa chaguo la kwanza katika timu yake mpya. Hivyo basi, Real Siciedad ya Uhispania ni chaguo bora kwake.

TAFSIRI NA : NDUNGI MAINGI

  • Tags

You can share this post!

Gor Mahia yazoa Sh2 milioni na tiketi ya soka ya CAF kwa...

Ushindani mkali vyuo vikuu vikiingia debeni leo