• Nairobi
  • Last Updated May 19th, 2024 8:50 AM
Mbappe na Messi watambisha PSG dhidi ya Nantes katika pambano la Ligi Kuu ya Ufaransa

Mbappe na Messi watambisha PSG dhidi ya Nantes katika pambano la Ligi Kuu ya Ufaransa

Na MASHIRIKA

KYLIAN Mbappe alifunga mabao mawili kutokana na krosi za Lionel Messi katika mchuano wa Ligi Kuu ya Ufaransa (Ligue 1) ulioshuhudia waajiri wao Paris Saint-Germain (PSG) wakikomoa Nantes 3-0 mnamo Jumamosi.

Wenyeji Nantes walikamilisha mechi hiyo wakiwa na wachezaji 10 pekee uwanjani baada ya Fabio kunako dakika ya 24 baada ya kumchezea Vitinha visivyo.

Bao la tatu la PSG lilijazwa kimiani na Nuno Mendes katika dakika ya 68. Mabao 10 kati ya 26 ambayo Mbappe amefungia PSG mwaka huu wa 2022 yamechangiwa na Messi.

PSG ambao ni mabingwa watetezi wa Ligue 1, sasa wanaselelea kileleni mwa jedwali kwa alama 16 sawa na Olympique Marseille. Miamba hao wanaonolewa na kocha Christophe Galtier wameshinda mechi tano na kupiga sare moja kutokana na mechi sita zilizopita za Ligue 1.

MATOKEO YA LIGUE 1 (Jumamosi):

Nantes 0-3 PSG

Auxerre 0-2 Marseille

Lyon 5-0 Angers

TAFSIRI NA: CHRIS ADUNGO

  • Tags

You can share this post!

Manchester United wapiga Arsenal breki kali EPL

Hatimaye Rais Kenyatta ampongeza mshindi wa kura za urais...

T L