• Nairobi
  • Last Updated May 19th, 2024 8:50 AM
Mbungo roho juu masogora wake wataliza KCB leo

Mbungo roho juu masogora wake wataliza KCB leo

Na ABDULRAHMAN SHERIFF

KOCHA wa Bandari FC, Andre Cassa Mbungo, (pichani)ameeleza matumaini ya wachezaji wake kujituma ili wapate ushindi watakapopambana na KCB FC kutoka Nairobi leo kwenye mechi ya Ligi Kuu ya FKF, itakayochezwa uwanja wa Mbaraki Sports Club.

Mbungo amesema wachezaji hao watahitajika kujituma zaidi ili waweze kuzoa pointi zote tatu, hasa baada ya kukosa kucheza mechi yoyote ya ligi kwa kipindi cha mwezi mmoja na siku tatu.“Nina imani kubwa ya timu yetu kupata ushindi ingawa mechi kama hiyo ambayo ni ya kwanza tangu mechi zisimamishwe ni tatizo kutabiri matokeo yake,” akasema mkufunzi huyo raia wa Rwanda.

Mbungo anaeleza kuwa kuna baadhi ya wachezaji ambao wanaendelea na matibabu kutokana na majeraha madogo ingawaje hakutaka kutawataja majina akisema kuwa huenda wakaruhusiwa kucheza na madaktari wao.

“Nitachukua uamuzi asubuhi ya Alhamisi kama wale ambao wamekuwa na majeraha madogo wataweza kucheza,” akasema.Alisema mechi kama hiyo haiwezi kutabirika kwani wachezaji wamekaa kipindi kirefu bila ya kucheza na kwamba mechi za kirafiki ni tofauti na zile za mashindano ama za ligi.

“Lakini nina imani kwa kuwa tuko nyumbani, tutafanya vizuri,” akasema Mbungo.Wakati wa mechi ziliposimamishwa kwa sababu ya corona kwa zaidi ya siku 45, timu hiyo ya Bandari iliweza kutingishika kwenye mechi zake za awali wakati soka liliporuhusiwa kuchezwa kwani ilichukua muda kiasi kabla ya timu hiyo kurudia hali yake ya kawaida.

Lakini kwa kuwa mechi ya leo itachezwa uwanja wa nyumbani, mashabiki wana matumaini makubwa ya kuishuhudia timu yao ikifanya vizuri na kuibuka na ushindi dhidi ya KCB.Mwisho

You can share this post!

Barcelona waaga UEFA katika hatua ya makundi baada ya...

Kocha wa AFC haendi popote- Shikanda

T L