• Nairobi
  • Last Updated May 6th, 2024 5:55 AM
Mkenya Akida na AC PAOK waaga Klabu Bingwa Ulaya baada ya kichapo

Mkenya Akida na AC PAOK waaga Klabu Bingwa Ulaya baada ya kichapo

Na GEOFFREY ANENE

AC PAOK anayochezea Mkenya Esse Akida imebanduliwa kwenye Klabu Bingwa Ulaya ya Wanawake baada ya kupoteza 4-0 dhidi ya Rangers ugani Katerini mjini Katerini, Ugiriki, Jumapili.

Wenyeji PAOK walikuwa bega kwa bega na wageni wao kutoka Scotland katika kipindi cha kwanza fainali hiyo ya shindano la pili la raundi ya kwanza.

Hata hivyo, mambo yalianza kuwaendea visivyo walipokubali nyavu zao kuchanwa na Nicola Docherty dakika tano tu baada ya kipindi cha pili kuanza.

Kibarua ya PAOK kilifanywa kuwa kigumu wakati Hannah Davison aliongeza bao la pili dakika ya 58.

Juhudi za miamba hao wa Ugiriki kujinasua kutoka minyororo ya kupoteza ziligonga mwamba pale beki wake Maria Gkouni Papaioannou alipojifunga dakika ya 70 kabla ya Lizzie Arnot kugonga msumari wa mwisho zikisalia dakika nne kipenga cha mwisho kilie.

PAOK iliingia fainali baada ya kulipua Swansea kutoka Wales 2-0 nayo Rangers ilizima Ferencvaros kutoka Hungary 3-1 katika nusu-fainali mnamo Agosti 18.

  • Tags

You can share this post!

Harry Kane atambisha Tottenham dhidi ya Wolves katika EPL

Wapigakura Mlima Kenya walivyotimua madiwani wengi

T L