• Nairobi
  • Last Updated April 28th, 2024 12:38 PM
Mkenya Ouna namba nne bora nchini Rwanda

Mkenya Ouna namba nne bora nchini Rwanda

Na JOHN KIMWERE

KOCHA wa zamani wa Wazito FC na Mathare United, Frank ‘Furo’ Ouna ameorodheshwa nafasi ya nne kwa wakufunzi bora kwenye soka la Ligi Kuu nchini Rwanda. Ouna alijiunga na Musanze FC mwaka jana baada ya kukwepa Mathare United.

Kulingana na gazeti la New Times la nchini humo, kocha huyo amejizolea umaarufu huo baada ya kuongoza klabu na kufanikiwa kung’ata APR inayoongoza ligi kuu pia kutoka nguvu sawa dhidi ya AS Kigali na Rayon Sport. Alipojiunga na klabu wapinzani wao hawakutarajia kama angeibuka kati ya wakufunzi bora kwenye kampeni za kipute hicho msimu huu.

Musanze FC wakati aliyowahi kufanya vizuri na kumaliza kati ya nafasi sita bora ilikuwa miaka kumi iliyopita. ”Tayari nimeona jinsi magazeti ya humu nchini yameandika kunishusu nami nashukuru inaashiria wazi kuwa makocha wa Kenya tunaweza kufanya makubwa katika mataifa ya kigeni,” kocha huyo alisema na kuongeza kuwa anashukuru wasaidizi wake maana bila wao hangefikiua ufanisi huo.

Mkenya huyo ameongoza Musanze FC kusajili ushindi wa mechi nane, kutoka nguvu sawa mara nane na kudondosha patashika sita. Kwenye jedwali ya kipute hicho, Musanze inashikilia nafasi ya saba kwa kutia kapuni alama 32, tano mbele ya Espoir F baada ya kila moja kupiga mechi 22. Kiyovu Sports inaongoza kwa alama 50, mbili mbele ya APR. Nayo Mukuru imezoa alama 38 na kufunga tatu bora.

You can share this post!

Barcelona yakomoa Levante na kuingia nafasi ya pili La Liga

Mshukiwa wa mkasa wa moto ulioangamiza watu sita...

T L