• Nairobi
  • Last Updated May 3rd, 2024 7:50 PM
Nahodha John McGinn kuendelea kuchezea Aston Villa hadi 2027

Nahodha John McGinn kuendelea kuchezea Aston Villa hadi 2027

Na MASHIRIKA

NAHODHA wa Aston Villa, John McGinn, ametia saini mkataba mpya utakaomshuhudia akiendelea kuchezea kikosi hicho cha Ligi Kuu ya Uingereza (EPL) hadi mwaka wa 2027.

Kiungo huyo raia wa Scotland mwenye umri wa miaka 28 alijunga na Villa mnamo 2018 baada ya kuagana na kikosi cha Hibernian.

Alifunga bao muhimu la ushindi mnamo 2019 dhidi ya Derby County na kusaidia Villa kupanda ngazi hadi EPL. Amekuwa sehemu muhimu ya kampeni za kikosi hicho tangu wakati huo.

McGinn alipokezwa utepe wa unahodha kambini mwa Villa mnamo 2022-23 na akachezea kikosi hicho mara 36 katika mashindano yote mnamo 2022-23.

McGinn sasa anajiandaa kuongoza Villa kwenye kampeni za kwanza za soka ya bara Ulaya kwa mara ya kwanza tangu 2010-11 baada ya kikosi hicho kufuzu kwa kipute cha Europa Conference League.

Amechezea Villa mara 184 na kufungia kikosi hicho mabao 17.

TAFSIRI NA: CHRIS ADUNGO

  • Tags

You can share this post!

Pasta Ezekiel aandaa maombi maalum kubariki tawi jipya

Thika Queens sasa yamilikiwa na Police FC

T L