• Nairobi
  • Last Updated May 18th, 2024 10:55 AM
Napoli wajinasia huduma za Tanguy Ndombele kutoka Tottenham

Napoli wajinasia huduma za Tanguy Ndombele kutoka Tottenham

Na MASHIRIKA

KIUNGO mahiri wa Ufaransa, Tanguy Ndombele, 25, amejiunga na Napoli ya Ligi Kuu ya Italia (Serie A) kwa mkopo kutoka Tottenham Hotspur ya Uingereza.

Kwa mujibu wa maelewano, Napoli watakuwa huru kumpokeza sogora huyo mkataba wa kudumu jijini Naples mwishoni mwa msimu huu wa 2022-23 kutegemea matokeo yake.

Nyota huyo alichezea Olympique Lyon ya Ufaransa kwa mkopo mnamo 2021-22. Aliingia katika sajili rasmi ya Spurs mnamo Julai 2019 kwa Sh6.5 bilioni na akafungia kikosi hicho mabao 10 kutokana na mechi 91.

Napoli tayari wamelipa Spurs ada ya Sh102 milioni kwa ajili ya kufanikisha uhamisho wa Ndombele.

TAFSIRI NA: CHRIS ADUNGO

  • Tags

You can share this post!

Man-United wafungulia mifereji ya fedha na kumsajili...

Welbeck sasa kuchezea Brighton hadi Juni 2024

T L