• Nairobi
  • Last Updated May 18th, 2024 6:55 AM
Welbeck sasa kuchezea Brighton hadi Juni 2024

Welbeck sasa kuchezea Brighton hadi Juni 2024

Na MASHIRIKA

FOWADI Danny Welbeck, 30, sasa atachezea Brighton hadi Juni 2024 baada ya kutia saini mkataba mpya uwanjani Amex.

Mshambuliaji huyo wa zamani wa Manchester United na Arsenal, aliibuka wa tatu katika orodha ya wafungaji bora wa Brighton mnamo 2021-22 baada ya kupachika wavuni mabao sita.

Welbeck aliyechezea timu ya taifa ya Uingereza mara 42 kati ya 2011 na 2018, amewajibishwa na Brighton mara 53 na kufunga mabao 12 tangu Oktoba 2020.

“Ni mchezaji wa haiba kubwa ambaye atasalia tegemeo letu katika safu ya mbele. Ana kiu ya kushinda kila mechi na kielelezo chema kwa chipukizi wetu kambini,” akasema kocha wa Brighton, Graham Potter.

TAFSIRI NA: CHRIS ADUNGO

  • Tags

You can share this post!

Napoli wajinasia huduma za Tanguy Ndombele kutoka Tottenham

Arsenal yaendea AFC Bournemouth

T L