• Nairobi
  • Last Updated May 2nd, 2024 6:39 PM
PSG wapoteza mechi kwa mara ya kwanza tangu Machi 2022

PSG wapoteza mechi kwa mara ya kwanza tangu Machi 2022

Na MASHIRIKA

PARIS Saint-Germain (PSG) walipoteza mechi ya Ligi Kuu ya Ufaransa (Ligue 1) kwa mara ya kwanza tangu Machi 2022 baada ya Lens kuwapokeza kichapo cha 3-1.

Lens wanaokamata nafasi ya pili jedwalini wamepoteza mechi moja pekee kati ya 17 zilizopita za Ligue 1 na sasa wanajivunia alama 40, nne pekee nyuma ya PSG ya kocha Christophe Galtier inayoselelea kileleni mwa jedwali ikiwa na idadi kubwa ya wanasoka nyota.

Lois Openda alifunga bao na kuchangia jingine ambalo Lens ya Franck Haise ilifungiwa na Alexis Claude-Maurice mwanzoni mwa kipindi cha pili. Wenyeji Lens waliwekwa kifua mbele na Przemyslaw Frankowski kutokana na masihara ya kipa Gianluigi Donnarumma aliyetema.

PSG waliokosa huduma za Lionel Messi na Neymar Jr, walifutiwa machozi na Hugo Ekitike.

Japo Lens walitoka sare na Nice wiki iliyopita baada ya kipute cha Ligue 1 kurejelewa baada ya Kombe la Dunia, kikosi hicho kimeshinda mechi sita kati ya nane zilizopita ligini na tisa katika mashindano yote katika uwanja wao wa nyumbani muhula huu.

Kichapo cha mwisho kwa PSG kupokea ni cha 3-0 kutoka kwa AS Monaco mnamo Machi 20, 2022, siku 10 baada ya Real Madrid kuwakung’uta kwenye Klabu Bingwa Ulaya (UEFA).

TAFSIRI NA: CHRIS ADUNGO

  • Tags

You can share this post!

MAKALA MAALUM: Kimojawapo cha vivutio 2023 ni ulainishaji...

Biashara ya miraa yanoga nchini Somalia uzalishaji...

T L